TIMU ya taifa ya soka
Tanzania, ‘Taifa Stars’ inayojiandaa kwa ajili ya mchezo wa kuwania kufuzu kwa
Kombe la Afrika (AFCON), dhidi ya Msumbiji utakaopigwa Februari 29, imemuweka katika wakati mgumu Kocha wa Simba,
Mserbia Milovan Cirkovic, katika maandalizi yake ya mchezo wa marudiano dhidi
ya Kiyovu ya Rwanda.
Mchezo huo wa marudiano wa Kombe la Shirikisho
Afrika (CAF), unatarajiwa kupigwa Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam, kati ya
Machi 3-4 mwaka huu, baada ya ule wa awali uliopigwa Kigali mwishoni mwa wiki
na kumalizika kwa sare ya bao 1-1.
Ofisa Habari wa Simba Ezekiel Kamwaga amesema ugumu huo kwa Milovan, unatokana na kulazimika kupangua
programu zake za mazoezi yanayoanza leo, baada ya nyota wake tisa kuitwa Stars.
Alisema nyota wao waliobaki baada ya wale wa
Stars ni 18, ambao leo wataanza mazoezi baada ya kupumzika siku mbili.
Wachezaji wa Simba
walioitwa Stars, ambayo jana ilianza kambi ni Jonas
Gerald, Juma Kaseja, Masoud Cholo, Juma Nyoso, Juma Jabu, Kelvin Yondani,
Shomari Kapombe, Mwinyi Kazimoto na Uhuru Selemani.
Comments
Post a Comment