SIMBA WAREJEA DIMBANI, KUNOLEWA NA AZAM KESHO

MABINGWA wa kombe la Mapinduzi Azam FC kesho watashuka katika dimba lao la Chamazi lililopo Mbagala Dar es Salaam kuikaribisha Simba.
Mechi hiyo ni mahususi kwa kuipa makali Simba ambayo ipo katika maandalizi ya mechi yake ya marudiano ya kombe la Shirikisho dhidi ya Kiyovu ya Rwanda itakayopigwa wiki ijayo jijini Dar es Salaam.
Katika hatua nyingine Simba iliyokuwa katika programu ya kufanya mazoezi ya viungo sasa imeshamaliza ambapo wameanza mazoezi ya uwanjani katika viwanja vya TCC Chang'ombe, jijini Dar es Salaam.

Comments