Machi 8 kila mwaka ni Siku ya Wanawake
Dunia. Ili kuadhimisha siku hiyo kwa upande wa mpira wa miguu, TFF kwa
kushirikiana na Chama cha Mpira wa Miguu cha Wanawake (TWFA) imeandaa mashindano
mafupi kwa shule nane za sekondari za Mkoa wa Dar es Salaam.
Mashindano yataanza Februari
24 mwaka huu kwenye viwanja viwili vya Jitegemee Sekondari ambapo kutakuwa na
kundi B wakati kundi A litacheza mechi zake Makongo Sekondari. Mechi zitaanza
saa 8 mchana na kumalizika saa 10 jioni.
Kundi A lina shule za Makongo, Goba, Twiga
na Lord Barden wakati Jitegemee, Benjamin Mkapa, Kibasila na Tiravi zitakuwa
kundi B.
Lengo la mashindano ni
kuhamasisha mpira wa miguu kwa wasichana katika ngazi ya shule, kuandaa, kubaini
na kuendeleza mafanikio yanayopatikana katika timu ya wanawake ya
Taifa.
Pia kutoa fursa kwa watoto wa
kike kusherehekea Siku ya Wanawake duniani kupitia mpira wa miguu, kutekeleza
ushiriki wa TFF katika shughuli za kijamii na ni sehemu ya mchakato wa kuandaa
mashindano ya ligi kwa wasichana.
Uchaguzi wa timu shiriki
umezingatia mchango wa shule katika kuendeleza mpira wa miguu kwa
wasichana/wanawake. Pia zawadi zitatolewa kwa mshindi wa kwanza, pili na
tatu.
Mwenyekiti wa Kamati ya
Maandalizi ya Mashindano hayo ni Zainab Mbiro kutoka Twiga Sekondari wakati
wajumbe ni Brighton Mbasha (Jitegemee), Yusuf Mohamed (Tiravi),
Michael Bundala (TFF), Furaha Francis (TFF/TWFA) na Rose Kissiwa (TWFA).
Tunaomba wadau mbalimbali
wajitokeze kusaidia gharama za uendeshaji wa mashindano hayo.
Comments
Post a Comment