Mkurugenzi wa Lino Agency ambayo inaratibu shindano la Miss Tanzania, Hashim Lundenga aklizungumza na waandishi wa habari leo kuhusiana na udhamini mpya wa mashindano hayo, katikati ni meneja masoko wa kampuni ya bia Tanzania (TBL) Fimbo Butallah na kulia ni meneja wa kinywaji cha Redd's, Victoria Kimaro.
Butallah akifafanua jambo kwa waandishi wa habari leo
Meneja wa Redd's Victoria Kimaro akifafanua jambo kwa waandishi wa habari leo, kulia ni Miss Tanzania 2011/2012 Salha Israel
Mkataba unasainiwa Lundenga akishuhudiwa na mwenyekiti wa kamati ya Miss tanzania Prashant Patel na Victoria Kimaro
Kila kitu kimo ndani ya hayo makaratasi
Waandishi wa habari kazini Dina, Mwani na Vicky Kimaro
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Toleo la Leo
REDD’S ORIGINAL MDHAMINI
MKUU WA MISS TANZANIA 2012.
Dar es Salaam, FEBRUARY
15, 2012:
Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) kupitia kinywaji chake cha Redd’s Original leo imetangaza rasmi kuchukua nafasi ya “Mdhamini Mkuu” wa
shindano kubwa kabisa la urembo hapa nchini lijulikanalo kama “Miss Tanzania”.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es salaam, meneja masoko wa
TBL Bw. Fimbo Butallah alisema; Redds Original, leo inatangaza kuwa ndio
wadhamini wakuu wa mashindano ya urembo Tanzania, yanayojulikana kama “Miss
Tanzania”. Kwa udhamini huu, mashindano haya sasa yatajulikana kama “REDDS MISS TANZANIA 2012”. Kwa miaka
kadhaa sasa Redds Original imekuwa ikishiriki katika mashindano haya kama
mdhamini mwenza, yaani “Kinywaji rasmi cha Miss Tanzania”. Hivyo leo tunapiga
hatua nyingine kubwa katika historia ya tasnia hii ya urembo hapa nchini kwa
kuwa mdhamini mkuu wa mashindano ya Miss Tanzania.
Katika kuonesha kuwa Redds Original, imedhamiria kwa dhati kuendeleza
tasnia hii, leo tumesaini mkataba wa udhamini wa mashindano haya kwa kipindi
cha miaka mitatu, yaani 2012 hadi 2014. Hii inawahakikishia wapenzi na
mashabiki wa mashindano haya kuwa wataendelea kushuhudia mashindano haya na
kuburudika na kinywaji cha Redds Original kwa kipindi chote hiki. Alisema
Butallah.
Nae Meneja wa Kinywaji cha Redds Original Bi. Victoria Kimaro alisisitiza
juu ya udhamini wa mashindano haya kuanzia ngazi za chini hadi ngazi ya Taifa.
Udhamini huu mkubwa wa mashindano ya Miss Tanzania unajumuisha udhamini
tutakaotoa katika maeneo mbali mbali kwa ngazi za vitongoji hadi Taifa.
Tunawaahidi mashabiki wote wa mashindano haya na wadau wa tasnia ya urembo
kujiandaa kwa burudani ya hali ya juu.
Akizungumzia udhamini huo, Mkurugenzi wa LINO Agency waandaaji wa shindano
la Miss Tanzania, Bw. Hasim Lundenga alisema; Kwa niaba ya kamati ya Miss
Tanzania napenda kutoa shukurani za dhati kwa TBL kupitia kinywaji chake cha
Redds Original kwa udhamini huu, na tunatangaza rasmi kuwa mashindano haya sasa
yataitwa “Redds Miss Tanzania’. Kitu kikubwa tunachowashukuru wadhamini wetu ni
mkataba ambao tumesaini hii leo, ukituhakikishia udhamini wa mashindano haya
kwa miaka mitatu.
Kwa mara nyingine tunawapongeza zaidi Redds original kwa kuwa mstari wa
mbele katika kuendeleza tasnia hii ya urembo hapa nchini. Tumekuwa nao bega kwa
bega kwa miaka kadhaa sasa, na haiwezekani ukazungumzia tasnia ya urembo hapa
nchini bila kuitaja Redds Original. Alisema Lundenga.
Comments
Post a Comment