MKUU wa Mkoa wa Dar es
Salaam ameifutia aibu klabu kongwe ya Yanga ya jijini Dar es Salaam baada ya
hafla maalumu ya kuichangia katika maadhimisho ya miaka 77 tangu kuanzishwa
kwake kudoda kwenye Hoteli ya Peacock.
Katika hafla hiyo
iliyokuwa imepangwa kuanza majira ya saa 1:00, uongozi wa Yanga uliwaalika
wadau mbalimbali wakiwamo viongozi wa serikali na wafanyabiashara wakubwa,
lakini mahudhurio yalikuwa hafifu.
Hadi muda wa kuanza
shughuli habari za uhakika kutoka ndani ya klabu hiyo zinaeleza kuwa
kulikuwa hakuna hata kiongozi mmoja, isipokuwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam , Saidi Meck Sadiki, ambaye
alikuwa mgeni rasmi.
“Yaani RC aliingia
ukumbini kama saa 1:30 hivi, lakini kulikuwa
hakuna kiongozi hata mmoja, hivyo kuonekana mgeni rasmi ndiyo mkaribisha wageni,”
kilisema chanzo hicho na kuongeza:
“Kutokana na maandalizi
hafifu ambayo hayaendani na miaka 77 ya Yanga, mbali na RC, viongozi wengine
wakamwalika Naibu Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Dk. Fenella
Mukangara, hivyo mambo kuzidi kuingiliana.
Inaelezwa kuwa hali
ilizidi kuwa mbaya wakati mnada wa vitu mbalimbali ulipoanza ambapo kutokana na
walengwa wengi kuingia mitini, mauzo yalidoda, hadi pale RC Sadiki, alipookoa
jahazi kwa kununua picha ya Rais wa Kwanza wa Zanzibar , Abeid Amani Karume kwa sh
1,750,000.
“Yaani si viongozi wala
hao walioalikwa, hakuna chochote walichokifanya, yaani ni aibu aibu, walileta
jezi kibao lakini hakuna aliyenunua zaidi ya jezi tatu kwa sh laki moja kila
moja,” alisema mtoa habari huyo na kubainisha kuwa
Kamati ya Utendaji ndiyo
kila kitu Yanga, lakini viongozi hawakupewa taarifa juu ya suala hilo na wao hawakuelewa
chochote, ndiyo maana walikuwa wanashangaa tu.
“Yaani bila ya Mkuu wa
Mkoa Saidi Meck Sadiki ambaye alitarajiwa kuwa mgeni rasmi katika hafla hiyo kununua
picha ya aliyekuwa Rais wa awamu ya kwanza wa Zanzibar , Abeid Amani Karume, ingekuwa aibu
tupu,” alisisitiza.
Mwisho
Comments
Post a Comment