Hatua ya fainali ya Ligi Daraja la Kwanza
(FDL) itafanyika kuanzia Machi 17 mwaka huu katika kituo ambacho kitatangazwa
baadaye.
Timu tatu kutoka katika kila kundi ndizo
zitakazocheza fainali hiyo. Washindi watatu wa juu ndiyo watakaofuzu kucheza
Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) msimu ujao.
Mikoa mitatu ya Mbeya, Mwanza
na Ruvuma imewasilisha maombi ya kuwa wenyeji wa fainali hizo. Maombi hayo
yanafanyiwa uchambuzi kabla ya kutangaza mkoa uliopewa nafasi hiyo.
Wakati huo huo, michuano ya
Ligi Daraja la Kwanza (FDL) hatua ya makundi inamalizika kesho (Februari 22
mwaka huu) kwa mechi tatu za kundi A.
Polisi Dar es Salaam watakuwa
wenyeji wa Morani FC ya mkoani Manyara katika mechi itakayochezwa Uwanja wa
Mabatini ulioko Mlandizi mkoani Pwani.
Mgambo Shooting Stars ya
Tanga itaoneshana kazi na Temeke United ya Dar es Salaam katika mchezo
utakaofanyika Uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga wakati Uwanja wa Jamhuri mjini
Morogoro utashuhudia mechi kati ya wenyeji Burkina Faso na Transit Camp ya Dar
es Salaam.
Boniface
Wambura
Ofisa
Habari
Shirikisho la
Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)
Comments
Post a Comment