FAINALI LIGI SOKA DARAJA LA KWANZA KUANZA MACHI 17


Hatua ya fainali ya Ligi Daraja la Kwanza (FDL) itafanyika kuanzia Machi 17 mwaka huu katika kituo ambacho kitatangazwa baadaye.
 
Timu tatu kutoka katika kila kundi ndizo zitakazocheza fainali hiyo. Washindi watatu wa juu ndiyo watakaofuzu kucheza Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) msimu ujao.
 
Mikoa mitatu ya Mbeya, Mwanza na Ruvuma imewasilisha maombi ya kuwa wenyeji wa fainali hizo. Maombi hayo yanafanyiwa uchambuzi kabla ya kutangaza mkoa uliopewa nafasi hiyo.
 
Wakati huo huo, michuano ya Ligi Daraja la Kwanza (FDL) hatua ya makundi inamalizika kesho (Februari 22 mwaka huu) kwa mechi tatu za kundi A.
 
Polisi Dar es Salaam watakuwa wenyeji wa Morani FC ya mkoani Manyara katika mechi itakayochezwa Uwanja wa Mabatini ulioko Mlandizi mkoani Pwani.
 
Mgambo Shooting Stars ya Tanga itaoneshana kazi na Temeke United ya Dar es Salaam katika mchezo utakaofanyika Uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga wakati Uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro utashuhudia mechi kati ya wenyeji Burkina Faso na Transit Camp ya Dar es Salaam.
 
 
Powered by Sorecson : Creation de site internet
Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)

Comments