MSANII wa muziki wa bongo fleva nchini Joseph Haule 'Prof J', amewataka Watanzania kuweka utaifa mbele kwa kuishangilia Yanga
katika mchezo wake na Zamelek utakaopigwa Februari 18 mwaka huu.
J alisema
siku hiyo Watanzania wanapaswa kujitokeza
kwa wingi huku wakiungana kwa pamoja kutoa sapoti kwa wachezaji wa Yanga kwa
kuwa wanaiwakilisha Taifa.
“Mimi mmoja wa mashabiki wa Simba lakini siku hiyo nitatoa
sapoti kwa timu ya nyumbani Yanga kwani
utaifa ni muhimu kuliko kitu kingine”alisema Prof J
Prof. J alisema kwa kufanya hivyo itakuwa ni hatua moja mbele
katika kufanya mapinduzi ya maendeleo ya
mchezo huo unaopendwa na wengi hapa nchini.
Alisema ushabiki wa kuzizomea timu za hapa nyumbani
zinapocheza na wageni hausaidii kuinua kiwango cha soka na kuliletea Taifa
mafanikio bali unazindi kurudisha nyuma mafanikio yanayotarajiwa.
Prof J alisema Watanzania ni muhimu wakaweka utaifa mbele kwa
kuzishangilia timu zao kwa kuwa kila timu inaposhinda ni taifa ndilo linalopata
heshima na kutambulika katika mchezo huo duniani.
Comments
Post a Comment