CHELSEA YAUA 3-0 ENGLAND

LONDON, England
KLABU ya Chelsea jana iliibuka na ushindi waq mabao 3-0 dhidi ya Bolton na kufanikiwa kurejea ndani ‘top four’ kwenye Ligi Kuun ya England sambamba na kumpunguzia jakamoyo kocha wake, Andre Villas-Boas.
Shukrani kwao David Luiz, Didier Drogba na Frank Lampard kwa mabao yao ya kipindi cha pili yaliyozimja gundu la Chelsea kucheza mechi tano bila kushinda, hali ambayo ilikuwa inakiweka matatani kibarua cha kocha Villas-Boas.
Ushindi huo unaifanya klabu hiyo ya London ipande nafasi ya nne, juu ya Arsenal.
Bolton wanabaki kwenye ‘maeneo’ ya kushuka na wameshindwa kuvunja mwiko wa kutoifunga Chelsea tangu mwaka 2003.

Comments