ZH POPE YABEBA WAAMUZI WA MECHI YA TWIGA STARZ

Kampuni ya ZH Hope Limited imegharamia tiketi za waamuzi na kamishna atakayesimamia mechi ya mchujo kuwania tiketi ya kucheza fainali za Afrika kwa Wanawake (AWC) kati ya Tanzania (Twiga Stars) na Namibia itakayofanyika Januari 29 mwaka huu jijini Dar es Salaam.

Mbali ya tiketi hizo za ndege, pia kampuni hiyo itagharamia hoteli (malazi na chakula) kwa kamishna na waamuzi hao wanne kwa muda wote watakaokuwepo nchini kwa ajili ya mechi hiyo.
Gharama za tiketi na hoteli kwa kamishna wa mechi hiyo na waamuzi hao watakapokuwa hapa nchini ni sh. 11,856,000.
Bajeti nzima ya mechi hiyo ni sh. 74,660,000. Hiyo inajumuisha usafiri, posho kwa wachezaji, posho kwa benchi la ufundi, gharama za kambi, dawa na maji ya kunywa wakati wa mazoezi na mechi kwa Twiga Stars. Maeneo mengine usafiri wa ndege, usafiri wa ndani (magari mawili), posho na hoteli kwa kamishna na waamuzi.

Gharama nyingine za timu ya Namibia itakayokuwa na watu 25 ambazo ni usafiri wa ndani (magari matatu), hoteli (malazi na chakula) na maji ya kunywa wakati wa mazoezi na mechi.



Comments