Zambia na Libya jana Jumatano zilitoka sare ya 2-2 katika mechi ya iliyochezwa katika uwanja uliokuwa umeloa maji
Mkwaruzano huo ulicheleweshwa kwa karibu saa moja nzima kutokana na uwanja kujaa maji yalisababishwa na mvua kubwa inayonyesha eneo hilo.
Kabla ya kwenda mapumzikoni mshambulizi wa Libya Ahmed Saad Osman aliifungia nchi yake magoli mawili.Na katika kipindi cha pili Emmanuel Mayuka aliiwafungia vijana wa Chipolopolo bao la kwanza na halafu Christopher Katongo akafanya mambo kuwa 2-2.
Kabla ya hapo mechi hiyo ya kundi A ilionekana kama ingeliahirishwa kutokana na mvua kubwa iliyokuwa ikinyesha.
Comments
Post a Comment