WAZIMBABWE KUICHEZESHA TWIGA STARS v NAMIBIA, MECHI YAO KUONESHWA LIVE


Mechi ya marudiano kusaka tiketi ya kucheza fainali za Nane za Kombe Afrika kwa Wanawake (AWC) zitakazofanyika Novemba mwaka huu nchini Equatorial Guinea kati ya Tanzania (Twiga Stars) na Namibia itachezeshwa na waamuzi kutoka Zimbabwe.
Waamuzi katika mechi hiyo itakayofanyika Januari 29 mwaka huu Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam watakuwa Rusina Majo Kuda (mwamuzi wa kati) wakati waamuzi wasaidizi ni Stellah Ruvinga na Rudo Nhananga. Mwamuzi wa akiba ni Pamela Chiwaya. Kamishna wa mechi hiyo ni Beletsh Gebremariam kutoka Ethiopia.

MECHI YA TWIGA STARS KUONESHWA ‘LIVE’

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limekipa Kituo cha Televisheni cha ITV haki ya kipekee (exclusive rights) kuonesha moja kwa moja (live) mechi kati ya Twiga Stars na Namibia itakayochezwa kuanzia saa 10 kamili jioni kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Twiga Stars ambayo tayari imeingia kambini Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) kambi ya Ruvu iliyoko Mlandizi mkoani Pwani iwapo itafanikiwa kuitoa Namibia itafuzu kucheza raundi ya kwanza na mshindi kati ya Misri na Ethiopia. Twiga Stars ilishinda mechi ya kwanza ugenini mabao 2-0.

Boniface WamburaOfisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)

Comments