VIONGOZI WA MICHEZO NA WADAU WAMUAGA MAREHEMU REGIA MTEMA

 WAZIRI wa habari utamaduni na Michezo Dkt. Emmanuel Nchimbi (mwenye miwani) aikuaga mwili wa mbunge wa Viti maalum (CHADEMA), Regia Mtema katika Viwanja vya Karimjee, jijini Dar es Salaam leo.
 Mwenyekiti wa Simba ambayo Alhaj Ismail Aden Rage (suti) nyeupe naye alikuwa mmoja ya walioshiriki kuaga mwili wa marehemu Regia Mtema ambaye anatarajiwa kuzikwa kesho Ifakara, pembeni mwa Rage (kulia) ni aliyekuwa Mwenyekiti wa kamati ya Uchaguzi ya Yanga, Jaji Mkwawa.
 Naibu Katibu Mkuu wa CHADEMA ambaye pia ni mjumbe wa kamati ya fedha ya Simba, Zitto Kabwe akimkumbatia pacha wa  marehemu Regia, Kulwa  Mtema katika zoezi la kuaga mwili wa pacha mwenzake Regia (DoTo)ambaye pia alikuwa mwanachama wa Wekundu wa Msimbazi, Simba.
 Ujumbe huo !
Mbunge wa Mbeya mjini (CHADEMA) ambaye pia ni msanii wa hip hop nchini, Joseph Mbilinyi 'Mr.11' naye pia alikuwemo.
MWENYEZI MUNGU AIPUMZISHE ROHO YA MAREHEMU PEMA PEPONI, AMIN.

Comments

  1. YANGA BOMBA-UHURU BRANCHJanuary 18, 2012 at 6:32 AM

    Du poleni bwana kumbe dada alikua mnyama mwenzenu.Mungu amuweke mahala panapofaa inshallah.

    mdau wa bomba la uhuru,Revere,Masachusetts,USA

    ReplyDelete

Post a Comment