TFF YAMRUDISHA BASENA SIMBA


Malalamiko ya Kocha Moses Basena kwa TFF baada ya klabu yake ya Simba kusimamisha mkataba wake yaliwasilishwa mbele ya Kamati ya Sheria, Maadili na Hadhi za Wachezaji. 
Baada ya kupitia malalamiko hayo, uamuzi wa kamati ni kuwa suala hilo liendelee kuwa kati ya Simba na Basena na kuwataka wakae pamoja ili waweze kulipatia ufumbuzi. 
Licha ya Basena kuwa na mkataba wa miaka miwili na klabu hiyo, Kamati imebaini kuwa hauwezi kufanya kazi (functional) kwa vile kocha huyo hakuwa na kibali cha kufanya kazi nchini (work permit).
 Hivyo kisheria hakukuwa na mkataba kwa vile ili Basena aweze kuitumikia Simba ni lazima awe na kibali cha kufanya kazi nchini. TFF ilikataa maombi ya Simba kuiandikia barua Idara ya Uhamiaji kuthibitisha barua ya kumuombea work permit baada ya kocha huyo kushindwa kuwasilisha vyeti vyake vya ukocha. 
Kwa vile Simba imeshaajiri kocha mwingine (Milovan) kwa mkataba wa miezi sita na kupatiwa kibali cha kufanya kazi nchini, ufumbuzi wa suala la Basena unabaki kuwa kati ya klabu hiyo na kocha huyo.

Comments