KLABU ya soka ya Simba imetoa tahadhari kwa waamuzi watakaochezesha mzunguko wa pili wa ligi kuu bara kuwa makini na vitendo vya utovu wa nidhamu pamoja na kuumizwa wanavyofanyiwa wachezaji wao na wachezaji wa timu pinzani.
Ofisa Habari wa Simba Ezekiel Kamwaga
amesema kuwa wameaamua kutoa tahadhari mapema kwani katika mzunguko wa kwanza wachezaji wao wengi
waliumizwa kwa makusudi lakini waamuzi walishindwa kutoa adhabu ama onyo kwa
walioshiriki kufanya hivyo.
Alisema
kumeibuka tabia ya kuumiza wachezaji nyota na wale wa kigeni kwa lengo
la kuwa kufanya hivyo kutachangia kushusha ama kuhuisha viwango vyao
sambamba na kuizorotesha timu kwa namna moja ama nyingine.
Kamwaga alisema katika mzunguko wa kwanza wachezaji wao
wakiwemo Felix Sunzu, Gervais Kago waliumizwa kwa makusudi na mwamuzi
aliyekuwepo hakutoa adhabu yoyote.
Comments
Post a Comment