Mechi kati ya Toto Africans na African Lyon
ambayo kwa mujibu wa ratiba ilikuwa ichezwe Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza
haitakuwepo, na sasa itapangiwa tarehe nyingine.
Juzi Shirikisho la Mpira wa
Miguu Tanzania (TFF) lilipokea barua kutoka kwa wamiliki wa Uwanja wa CCM
Kirumba ikieleza kuwa Februari 5 mwaka huu uwanja huo utatumika kwa sherehe za
kitaifa za kuzaliwa Chama Cha Mapinduzi (CCM), hivyo hautaweza kutumika kwa
Februari 4, 5 na 6 mwaka huu.
Comments
Post a Comment