SHIRIIKISHO la Soka Tanzania (TFF) limesema kuwa mpaka sasa hakuna kituo cha
televisheni ambacho kimeomba na kushinda tenda ya kuonesha moja kwa moja (live)
mechi za Ligi Kuu ya Vodacom. Kwa upande wa vituo vya redio, vyote vimepewa haki
ya kutangaza moja kwa moja mechi za ligi hiyo kwa masharti
yafuatayo;
Kuitambulisha ligi hiyo kwa
jina lake (Ligi Kuu ya Vodacom) wakati wa matangazo hayo ya moja kwa moja, na
pia kuweka matangazo ya mdhamini (Vodacom) wakati wakitangaza mechi husika. Hata
hivyo, vituo vya redio bado vinaruhusiwa kuendelea kutafuta/kutumia matangazo ya
wadhamini wao, lakini ambao si washindani wa kibiashara wa Vodacom.
Comments
Post a Comment