MZUNGUKO WA PILI WA LIGI KUU BARA KUANZA J'MOSI KWA NYASI ZA VIWANJA VINNE KUWAKA MOTO



Mzunguko wa pili wa Ligi Kuu ya Vodacom kuwania ubingwa wa Tanzania Bara unaanza keshokutwa (Januari 21 mwaka huu) kwa mechi nne. Moro United itaikaribisha Yanga kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam na Mtibwa Sugar itaoneshana kazi na Oljoro JKT kwenye Uwanja wa Manungu, Turiani.
 
Nayo Toto Africans itakuwa mgeni wa Ruvu Shooting kwenye Uwanja wa Mlandizi mkoani Pwani na Villa Squad itapambana na Kagera Sugar katika Uwanja wa Azam Chamazi, Dar es Salaam.
 
Januari 22 mwaka huu JKT Ruvu na Polisi Dodoma zitapepetana Uwanja wa Azam Chamazi wakati Januari 22 mwaka huu Dar es Salaam itakuwa na mechi mbili; African Lyon na Azam (Uwanja wa Azam Chamazi) na Simba na Coastal Union (Uwanja wa Taifa).
 
Ratiba kwa ajili ya waamuzi na makamishna kwa mechi 35 za mwanzo tayari imeshatoka. Waamuzi wa kati 16 wameteuliwa kuchezesha mechi hizo huku watatu wakiwa wenye beji za Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA).

Makamishna ni 28 huku watathmini wa waamuzi (referees assessors) wakiwa kwenye mechi tano. Watathmini hao ni Charles Mchau, Soud Abdi, Emmanuel Chaula, Army Sentimea na Joseph Mapunda.

 

Comments

  1. YANGA BOMBA -UHURU BRANCHJanuary 19, 2012 at 10:39 PM

    UWE FASTA KUTUWEKEA MATOKEO,TENA YOTE SIO YA WANYAMA AU YANGA TU...SIE WENGINE TUKO MBALI NA TUNAKUTEGEMEA WEWE ZAIDI KWENYE MASUALA YA SOKA!

    MDAU WA YANGA BOMBA,REVERE,MASSACHUSSETTS

    ReplyDelete

Post a Comment