MZUNGUKO WA PILI VPL KUCHEZWA SIKU TATU KWA WIKI


Siku za mechi (match days) kwa Ligi Kuu ya Vodacom msimu wa 2011/2012 ambayo itaanza mzunguko wake wa pili Januari 21 mwaka huu sasa itakuwa ni Jumamosi, Jumapili na Jumatano tu.
 
Uamuzi huo umefanya na Kamati ya Ligi ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) iliyokutana Januari 5 mwaka huu ambapo pamoja na mambo mengine ilikuwa kupitia ratiba ya Ligi Kuu ya Vodacom na ile ya Daraja la Kwanza.
 
Kutokana na kituo cha Dar es Salaam kuwa na timu saba kati ya 14 za Ligi Kuu zinazotumia viwanja viwili tu (Uwanja wa Taifa na Uwanja wa Azam), kamati imepitisha uamuzi kuwa mechi mbili zinaweza kuchezwa kwa wakati mmoja (Taifa na Azam) ili ligi ichezwe ndani ya kalenda.
 
Timu zinazotumia viwanja hivyo kama vya nyumbani katika Ligi Kuu ya Vodacom ni African Lyon, Azam, JKT Ruvu Stars, Moro United, Villa Squad, Simba na Yanga.
 

Comments