Mwape (kulia) akiwa na mtoto wa Mamapipiro (Prince Akbar AKA Ince), kushoto ni kipa wa Yanga, Yaw Berko.
Na
Dina Ismail
WAKATI
uongozi wa klabu ya soka ya Yanga ukidai mshambuliaji wake wa Kimataifa Mzambia
Davies Musonda Mwape yu Mgonjwa, nyota huyo ameibuka na kudai yupo fiti kwa asilimia 100 ila hajisiki kucheza.
Akizungumza
na mwandishi wa habari hizi kutoka kutoka kwao zambia jana, Mwape alisema hana
majeruhi wala haumwi ila kisaikolojia hayupo fiti kwa asilimia 100
Mwape
ambaye hakuwa tayari kusema lini atarejea amekuwa tegemo katika safu ya
ushambuliaji tangu ajiunge na timu hiyo msimu uliopita.
Mshambuliaji
huyo wa zamani wa Orlando Poirates ndiye aliyefunga bao la pekee la ushindi
katika mechi ya watani Simba oktoba 31, 2011 kwenye Uwanja wa Taifa.
Lakini
tangu wamepewa likizo baada ya kumalizika kwa mzunguko wa kwanza hajajiunga na
timu yake huku uongozi ukidai anumwa nyama za paja.
Ofisa
habari wa Yanga, Louis Sendeu alisema jana kwamba Mwape bado anaumwa nyama za
paja na yupo kwao Zambia
akiendelea ku7jiuguza.
“Mimi
ninachofahamu Mwape ni mgonjwa na ametakiwa kujitibia majeruhi yake kutokana na
ukweli kwamb a amekuwa akiandamwa na matatizo haya kila mara,”Alisema.
Yanga
tayari ipo kambini ikijandaa na mzunguko wa pili wa ligi kuu bara na ligi ya mabingwa barani Afrika, michuano
ambayo wataanza na Zamalek ya Misri mwishoni mwa mwezi huu.
Kwa
sasa baadhi ya wachezaji wa Yanga wapo Zanzibar
katika kombe la Mapinduzi na wengine wapo jijini Dar es Salaam wakiendelea na mazoezi katika
Uwanja wa Loyoila.
Kutofautina
kwa kauli za Yanga na Mwape kunaashiria
kwamba kuna kitu kimejificha katika baina ya pande hizo mbili ambapo hakuna upande
uliokuwa tayari kukifichua.
mwisho
Comments
Post a Comment