MBUNGE
wa Ubungo (CHADEMA) John Mnyika (pichani)lkesho anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika
fainali za soka za kuwania kombe la Kinesi ukizikutanisha timu za Simba
B na Friends Rangers kwenye dimba la Kinesi, jijini Dar es Salaam.
Ofisa
habari wa Simba Ezekiel Kamwaga amesema kwamba timu yake
imejipanga vema kuhakikisha inashinda mchezo huo ambao utakuwa wa
kihistoria kwa timu hiyo.
“Kama
mnavyofahamu timu yetu haijawahi kufika fainali tangu kuanzishwa kwa
michuano hiii karibu miaka 20 hivyo kufika fainali tu ni jambo la
kihistoria…hivyo nawaomba wadau kujitokeza kwa wingi
kushuhudia,”Alisema.
Comments
Post a Comment