NYIMBO Mpya wa mwanamuziki mpya
wa bendi ya muziki wa dansi nchini Mashujaa Band Charles Gabriel, Charlz
Baba' umeanza kusika katika vyombo mbalimbali vya radio hapa nchini.
Akizungumza Dar es Salaam jana
Charlz Baba alisema hiyo ijulikanayo kama Ungenieleza ndiyo nyimbo yake
ya kwanza katika bendi hiyo ambayo anaamini itasikika na kukubalika kwa
wadau mbalimbali wa muziki hapa nchini.
Alisema licha ya kutoa kibao hicho anaharakati ya kutoa kitu
kingine ambacho ndani ya wiki mbili nacho kitakuwa tayari kuwa masikio
mwa watu.
Charlz Baba alisema ndani ya miezi mitatu ana uhakika wa nyimbo tatu kukamilika ikiwa na hata video zake kutengenezwa.
"Hiki cha kwanza yarai kipo kwenye radio kitaanza kukika hivi
karibuni na nina uhakika wadau wa muziki watakubali kazi yangu hii
ambayo nimeimba kwa kushirikiana na wanamuziki wenzangu wa Mashujaa
Band"alisema Charlz Baba.
Alisema wapo vizuri na wanamuziki wenzake wa bendi hiyo hivyo ana
uhakika wa bendi yao kufanya vizuri katika tasnia ya muziki wa dansi
hapa nchini.
Charlz Baba bendi yao kesho itakuwa ndani ya kumbi wao wa nyumbani wa Business Park Kijitonyama Dar es Salaam.
Comments
Post a Comment