Kwa mara nyingine mshambuliaji Mario Balotelli alijitokeza kua kiini cha mgogoro na sababu ya kuipatia Manchester city ushindi ikipiga hatua dhidi ya mshindani wake wa karibu Manchester United.
Habari kubwa kutoka mchuano huo hata hivyo haukua ushindi wa City bali gumzo lilizunguuka jinsi Balotelli alivyomkanyaga kichwani Scott Parker.
Harry Redknap aliwambia wandishi habari kua alishangazwa na jinsi refa alivyoshindwa kuliona kosa la Balotelli akimkanyaga Parker makusudi. Hivyo, Balotelli akaongezea umaarufu wake kwa mashabiki wa klabu yake wanaompenda licha ya wengi kuhusu ni juha katika soka ya England.
Comments
Post a Comment