YONDAN AJISALIMISHA MSIMBAZI

MCHEZAJI aliyezua utata ndani ya klabu ya Simba kwa muda mrefu Kelvin Yondan ametuliza mzuka na kurejea kundini ambapo amejiunga na wenzake wanaoendelea na mazoezi jijini Dar es Salaam.
Yondan ambaye amekuwa akiumiza vichwa vya viongozi kutokana na kuwa nje ya klabu hiyo kwa muda mrefu huku akidaiwa kuwa na mpango wa kujiunga na mahasi wao wa jadi, Yanga.
Hata hivyo uongozi wa Simba umeendelea kuwa na msimamo kuhusiana na suala la mchezaji huyo ambaye pamoja na kulimwa barua za kujieleza kwa mara kadhaa lakini alionekana kutoshtuka zaidi ya kuendelea kujichimbia anapoapajua mwenyewe.

Comments

Post a Comment