KIUNGO wa Ivory Coast Yaya Toure (28) ametawazwa kuwa mwanasoka bora wa Afrika kwa mwaka 2011 kupitia tuzo zilizotolewa na Shirikisho la Soka Barani Afrika (CAF) na kufanyika katika ukumbi wa Banquet uliopo ndani ya Ikulu ya Ghana.
Toure anayekipiga katika klabu ya Manchester City ya Uingereza alitwaa tuzo hiyo baada ya kupata kura nyingi na kuwapiku nyota wenzake aliotinga nao fainali, Mghana Andre Ayew na Seydou Keita wa Mali .
Mbali na tuzo hiyo pia kulitolewa tuzo mbalimbali kama ifuatavyo:
Mchezaji bora wa mwaka (anayekipiga Afrika):
-Oussama Darragi (Tunisia).
Mchezaji bora (Wanawake)
- Perpetua Nkwocha (Nigeria)
Mchezaji anayechipukia:
- Souleymane Coulibaly (Ivory Coast)
Mwamuzi bora:
-Noumandiez Doue (Ivory Coast)
Kocha Bora:
-Harouna Doula (Niger)
Timu bora ya Taifa (Wanawake):
-Cameroon
Klabu bora:
- Esperance ya Tunisia)
Nidhamu ya Mchezo:
-Libya
Tuzo ya Heshima:
-Mustapha Hadji( Morocco) na Austin ‘Jay-Jay’Okocha ( Nigeria)
Kiungo wa Ivory Coast, Yaya Toure (katikati), wa Manchester
City, akipokea tuzo ya Mwanasoka Bora Afrika 2011 mjini Accra, Ghana kutoka kwa
Mkurugenzi Mtendaji wa Globacom, Adewale
Shangowawa (kulia). Toure mwenye umri wa miaka 28, aliwapiku kiungo Mghana wa
Marseille, Andre Ayew (wa pili kushoto) na kiungo wa Mali na Barcelona, Seydou
Keita katika kura zilizoopigwa na makocha wea Afrika.
Comments
Post a Comment