MLINZI wa AC Milan Mario Yepes atakuwa nje kwa wiki kumi kufuatia maumivu ya kifundo cha mguu wake wa kulia ambayo yatamfanya afanyiwe upasuaji.
Yepes alipatwa na majeruhi hayo katika mechi baina ya AC MIlan na Bologna jumapili iliyopita na timu hizo kutoka sare ya mabao 2-2 na hivyo kutolewa kabla ya mchezo kumalizika.
Kwa mantiki hiyo walinzi wa nyuma ambao wataendelea kuliendesha jahazi Milan inayoshiriki ligi ya Seria A ikishika nafasi ya tatu ni pamoja na Alessandro Nesta, Thiago Silva na Philippe Mexes.
Comments
Post a Comment