TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
KLABU ya soka ya Simba ya Dar
es Salaam inatoa salamu za rambirambi kwa Shirika la Utangazaji Tanzania
(TBC) na tasnia ya habari kwa ujumla kufuatia kifo cha aliyekuwa mtangazaji
maarufu wa michezo nchini, Halima Mchuka, aliyefariki usiku wa kuamkia jana.
Jina la Halima Mchuka ni
maarufu kwa wanamichezo si Tanzania
pekee bali ukanda mzima wa Afrika Mashariki na Kati kwa vile yeye aliweka
historia ya kuwa mwanamke wa kwanza kutangaza mchezo wa soka redioni.
Katika enzi za uhai wake,
Halima alifanya kazi kwa karibu na klabu ya Simba, akitembelea ofisi za makao
makuu mtaa wa Msimbazi kwa ajili ya kutafuta taarifa mbalimbali za kimichezo.
Simba itaukumbuka daima
mchango wa Halima Mchuka kama mwanahabari,
mwanamichezo na mtu ambaye alivutia wanawake wengi kupenda mchezo wa soka na
pia kazi ya utangazaji na uandishi wa habari kwa ujumla.
Mwenyezi Mungu aiweke roho ya
marehemu mahali pema peponi. Amen.
Imetolewa na
Ezekiel Kamwaga
Ofisa Habari
Simba Sports Club
0772 01 72 47
Comments
Post a Comment