NORONGORO WAANZA KWA SARE COSAFA

Tanzania (Ngorongoro Heroes) imeanza kwa sare michuano ya Baraza la Vyama vya Mpira wa Miguu Kusini mwa Afrika (COSAFA) kwa vijana chini ya miaka 20 inayofanyika Gaborone, Botswana.
Jana (Desemba 2 mwaka huu) katika mchezo dhidi ya mabingwa watetezi Zambia uliofanyika Uwanja wa Chuo Kikuu cha Gaborone, timu hizo zilitoka sare ya kufungana mabao 3-3.
Mabao ya Ngorongoro Heroes yalifungwa dakika ya 2 na 13 kupitia kwa Simon Msuva. Bao la tatu lilifungwa na Hassan Dilunga dakika ya 40. Evans Kangwa aliifungia Zambia mabao mawili wakati la kusawazisha lilifungwa na Alex Sichone.
Ngorongoro iliwakilishwa na; Jackson Wandwi, Hassan kKessy, Issa Rashid, Samuel Mkomola, Frank Raymond, Atupele Jackson, Simon Msuva, Amani Kyata, Edward Shija, Frank Sekula na Hassan Dilunga.
Tanzania itacheza mechi ya pili Desemba 4 mwaka huu na Afrika Kusini wakati ya mwisho katika hatua hiyo ya makundi itakuwa Desemba 6 mwaka huu dhidi ya Mauritius.

Boniface Wambura Mgoyo
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)

Comments