MAN UTD WALALAIMIKIA TIKETI ZA MAN CITY

Manchester United imelalamika kwa Chama cha Kandanda cha England -FA- kuhusiana na mgao wao wa tikiti kwa mpambano wa Kombe la FA mzunguko wa tatu mwezi Januari dhidi ya Manchester City.
Uwanja wa Etihad mjini Manchester
Uwanja wa Etihad mjini Manchester

Chini ya taratibu za FA, Manchester United wana haki ya kupata mgao wa asilimia 15 ya uwezo wa viti 47,805 katika uwanja wa Etihad, ambao ni sawa na tikiti 7,100.
Hata hivyo, Manchester City imetoa tikiti 5,500, ikiwa ni asilimia 11 tu, hii ni kutokana na sababu za usalama uwanjani.
Manchester United ina mgawanyo maalum kutoka kwa FA, kutokana na uwezo wa uwanja wake wa Old Trafford wenye viti 76,000, kutoa asilimia 11 ya tikiti kwa timu ngeni, sawa na tikiti 8,500.
Mashateni hao Wekundu wanadai wapatiwe mgao wao kamili kwa ajili ya pambano hilo, litakaloanza saa saba mchana siku ya Jumapili tarehe 8 mwezi wa Januari.
Manchester City, ambao kwa sasa wanashikilia usukani wa Ligi Kuu ya England, watawakaribisha mahasimu wao hao wakubwa Manchester United katika mtanange huo wa Kombe la FA kwa mara ya kwanza tangu mwaka 1955.
Timu hizo zilikutana katika hatua ya nusu fainali mwaka jana kwenye Kombe la FA uwanja wa Wembley, ambapo Manchester City waliibuka washindi kwa bao 1-0 , baadae wakailaza Stoke katika fainali na kufanikiwa kushinda mashindano makubwa kwa mara ya kwanza kwa kipindi cha miaka 35.
Manchester City iliwaadhibu Man United walipokutana mara ya mwisho kwa mabao 6-1 katika mchezo wa Ligi Kuu ya England kwenye uwanja wa Old Trafford.

Comments