Shughuli ya usajili kwa ajili
ya timu za Tanzania zitakazoshiriki michuano ya ngazi ya klabu Afrika
inayosimamiwa na Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF)
inaendelea.
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)
Yanga itacheza Ligi ya
Mabingwa (CL) wakati Simba itashindana katika michuano ya Kombe la Shirikisho
(CC). Kwa upande wa Yanga hadi sasa imeshawasilisha Shirikisho la Mpira wa Miguu
Tanzania (TFF) majina ya wachezaji 28 wakati Simba majina 24 kwa ajili ya
usajili huo.
Mwisho wa kufanya usajili ni
Desemba 31 mwaka huu, na kila klabu inaruhusiwa kusajili hadi wachezaji 30. Hata
hivyo Agosti mwakani kutakuwa na usajili wa dirisha dogo kwa timu ambazo
hazikumaliza nafasi zote 30.
Kuna mifumo miwili ya
usajili; online (mfumo wa mtandao) au offline (kutuma fomu za usajili CAF kwa
njia ya DHL). TFF tumeamua kutumia mfumo wa online.
FIFA YAMTEUA MINJA KUSIMAMIA
MECHI
Shirikisho la Kimataifa la
Mpira wa Miguu (FIFA) limemteua Katibu wa Kamati ya Waamuzi ya TFF, Joan Minja
kuwa kamishna wa mechi ya Kombe la Dunia kati ya Zambia na
Botswana.
Mechi hiyo ya raundi ya awali
kwa ajili ya Fainali za Kombe la Dunia kwa Wasichana wenye umri chini ya miaka
17 zitakazofanyika mwakani nchini Azerbaijan itachezwa kati ya Februari 3, 4 au
5 mwakani jijini Lusaka.
Kwa upande wa Afrika nchi
ambazo zitacheza raundi ya awali ya michuano hiyo ni Afrika Kusini, Botswana,
Cameroon, Gambia, Ghana, Guinea, Namibia, Nigeria, Sierra Leone, Tunisia na
Zambia.
KOZI YA MAKAMISHNA KUANZA
KESHO
Kozi kwa ajili ya makamishna
wa mechi za Ligi Kuu na mashindano mengine yanayosimamiwa na Shirikisho la Mpira
wa Miguu Tanzania (TFF) inafanyika kesho (Desemba 28 mwaka huu) na keshokutwa
(Desemba 29 mwaka huu).
Washiriki wa kozi hiyo itakayofanyika ofisi
za TFF ni wale wanaoomba kwa mara ya kwanza (beginners), na waliokosa ile ya
awali iliyofanyika Agosti 6-8 mwaka huu. Pia ambao hawakufaulu katika kozi ya
awali wanayo fursa ya kushiriki ya sasa.
Washiriki wanatakiwa kuwa
waamuzi wastaafu na viongozi (administrators) wa mpira wa miguu katika ngazi
mbalimbali. Pia wanatakiwa kuwasilisha vyeti vyao halisi (original) vya
elimu.
Kutakuwa na mitihani ya
kuandika ya sheria za mpira wa miguu na picha (video clips). Kwa wanaotaka kuwa
makamishna ni lazima washiriki katika kozi ambapo ada ni sh.
10,000.
Makamishna waliofaulu kwenye kozi iliyopita
ni Abdallah Mitole, Amri Kiula, Arthur Mambeta, Charles Komba, Charles Ndagala,
David Lugenge, Edward Hiza, Fulgence Novatus, Gabriel Gunda, George Komba,
Godbless Kimaro, Hamis Kissiwa, Hamis Tika, James Mhagama, Jimmy Lengwe, Michael
Bundara, Mohamed Nyange, Mwijage Rugakingira, Omari Mwamela, Paul Opiyo, Pius
Mashera, Salim Singano, Victor Mwandike na William Chibura.
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)
Comments
Post a Comment