VIJANA WANACHAMA YANGA KUFANYA KONGAMANO DESEMBA 18

KONGAMANO maalum litakalowahusisha vijana wanachama na wasiowanachama wa klabu ya Yanga linatarajiwa kufanyika Desemba 18 katika ukumbi wa PTA, jijini Dar es Salaam, huku moja ya lengo lake kubwa mo kuweka nyasi bandia katika uwanja wa Kaunda.
Mjumbe wa kamati ya maandalizi na mratibu wa kongamano hilo, Kais Edwin alisema jana kwamba lengo la kongamano hilo ni kuwakutanisha vijana hao kwa ajili ya kutambua umuhimu na majukumu yao ndani ya klabu hiyo.
Alisema, kupitia kongamano hilo kutatolewa mada toka kwa wadau mbalimbali wakiwemo viongozi wa Yanga, wadau toka taasisi za kiserikali na zisizo za kiserikali ambapo maazimio yatakayopatikana watayawasilisha kwa viongozi wa klabu hiyo.
Aliongeza kuwa, wamepata baraka zote toka viongozi wa Yanga, Wanachama na hata viongozi wa serikali na baada ya kufanyika jijini Dar es Salaam litafanyika katika mikoa mingine, hivyo amewaomba walengwa kujitokeza kwa wingi.

Comments

  1. YANGA BOMBA-UHURU BRANCHNovember 22, 2011 at 6:35 PM

    KILA LA KHERI WANANGU WA BOMBA LA UHURU,NAONA MNAWAKILISHA VYEMA,SAFI SANA HAYO NDIO MABO YANAYOTAKIWA!

    ReplyDelete

Post a Comment