STARS KUTEMBELEA MAKUMBUSHO YA TAIFA KESHO, MA-PRO WAANZA KUWASILI

Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) ambayo hivi sasa iko kambini kujiandaa kwa mechi dhidi ya Chad, kesho (Novemba 5 mwaka huu) saa 5 asubuhi itatembelea Makumbusho ya Taifa.
Ziara yao ni ya kawaida, lakini pia kutakuwa na onyesho la Historia ya Soka Tanzania.
  Wachezaji ambao tayari wapo kambini hoteli ya New Africa ni Juma Kaseja, Godfrey Taita, Shabani Nditi, Hussein Javu, Juma Jabu, Ramadhan Chombo, Shomari Kapombe, Nurdin Bakari, Nadir Haroub, Juma Nyoso, Erasto Nyoni, Mrisho Ngasa, Mwadini Ally na Aggrey Morris.
  Idrisa Rajab wa Sofapaka ya Kenya tayari naye yuko kambini wakati wachezaji wengine kutoka nje wanatarajia kuwasili leo usiku. Wachezaji wa mwisho kutoka nje tunawatarajia kesho.

Comments