MICHUANO ya soka ya vijana chini ya miaka 20, ‘Uhai Cup’ imefikia tamati leo ambapo vijana wa Simba wamefanikiwa kutwaa ubingwa baada ya kufunga Azam FC kwa penalti 6-5, mchezo uliopigwa kwenye uwanja wa Karume jijini Dar es Salaam.
Katika mchezo huo zilimaliza dakika 90 bila kufungana na hata mwamuzi alipoongeza dakika 30 ambapo nazo zilimalika kwa sare tasa pia na ndipo kuamuliwa changamoto ya mikwaju ya penalti.
Mchezaji bora ni Ramadhani Singano wa Simba, kocha bora ni Suleiman Matola,mchezaji bora alikuwa Simon Mzava wa Azam, mwamuzi bora ni Juma Seifu, mfungaji bora Willian Luciana wa Simba,kipa bora ni Aishi Salum wa Azam.
Nafasi ya tatu imekwenda kwa timu ya Taifa ya Vijana chini ya miaka 17, (U-17) Sarengeti Boys waliyoipata baada ya kuifunga Toto African ya Mwanza mabao 2-1.
ANGALAU SASA KINA ADEN WAMEPATA TAJI MOJA TOKA WAINGIE MADARAKANI!
ReplyDelete