SIMBA YAMALIZA KILELENI MZUNGUKO WA KWANZA LIGI KUU BARA

SIMBA SC imemaliza mzungo wa kwanza leo wa ligi kuu soka Tanzania Bara ikiwa inaongoza ligi hiyo kwa pointi moja zaidi dhidi ya mabingwa watetezi, Yanga.


Hiyo inafuatia leo Simba kulazimisha sare ya mabao 3-3 dhidi ya Moro United katika mechi iliyopigwa Uwanja wa Azam uliopo Chamazi, hivyo kutimiza pointi 28 baada ya kucheza mechi 13.

Yanga nao wamejisogeza karibu na vinara hao baada ya kuifunga polisi Tanzania mjini Dodoma bao 1-0 na kutimiza pointi 27 baada ya kucheza mechi 13 pia.

Mechi nyingine ni Mtibwa Sugar dhidi ya African Lyon 2-2, Toto v Azam 1-1, Oljoro JKT iliifunga Villa Squad bao 1-0.

Comments

  1. YANGA BOMBA - UHURU BRANCHNovember 2, 2011 at 11:34 PM

    WANYAMA KULIKONI????BADO MKO KWENYE HANGOVER YA KIPIGO CHA JUMAMOSI NAONA BADO MNAPEPESUKA..POLENI SANA

    ReplyDelete
  2. Hivi wewe DADA kwa nini upendi kuandika habari za YANGA.... TUAMBIE ILI TUJUWE KAMA HII BLOGU YAKO NI YA SIMBA...TU..TUMECHOKA KUFUNGUA BLOGU YAKO KUKUTA UPANDE MMOJA TU..,, INAAMAANA NA WEWE BADO KUFUNGWA NA YANGA KUNA KUUMA? KUMBUKA HIZI HABARI SISI TULIYO MBALI NDIO TUNATAKIWA TUZIPATE VIZURI ZAIDI...SIO KUANDIKA TU.. HAPO KICHWA CHA HABRI KILITAKIWA KIWE YANGA YAPUNGUZA GEPU....ONDOA MAPENZI ILI BLOGU YAKO IZIDI KUFAHAMIKA ZAIDI.. KUMBUKA SIMBA NA YANGA NDIYO ZENYE WAPENZI WENGI..NI BORA UWE UNAWEKA USAWA KOTE...NI HAYO...KWA USHAURII....ILA POLE S SAANA SISI SERIKALI NDIO TUNAKAMATA UKINGO SASA HIVI..NASIKAIA MMESHAAANZA KUMTAFUTA MCHAWI..POLENI SIMBAAAAAA

    ReplyDelete
  3. Dada Dina nakubaliana na mdau hapo juu, labda blog yako ungeandika blog ya Simba...ukweli ni kuwa nilikuwa nafungua blog yako kila siku, lakini siku hizi naona bora niende kwa Shaff and Aboood blog...I real do!

    Mdau juu kasema kila kitu,

    Mdau
    USA

    ReplyDelete

Post a Comment