SIMBA, MORO UNITED WAINGIZA MIL.5 CHAMAZI

Mechi namba 86 ya Ligi Kuu ya Vodacom kati ya Moro United na Simba iliyochezwa Novemba 2 mwaka huu Uwanja wa Azam ulioko Chamazi, Dar es Salaam imeingiza sh. 5,764,000.
Watazamaji waliokata tiketi kushuhudia mechi hiyo walikuwa 1,688 ambapo kiingilio kilikuwa sh. 10,000 kwa VIP na sh. 3,000 kwa majukwaa mengine. Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) ambayo ni asilimia 18 iliyolipwa ni sh. 879,254.
Gharama za awali kabla ya mchezo; kila klabu ilipata sh. 118,160 wakati Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) kilipata sh. 101,280 kutoka mfuko wa jichangie ambayo ni sh. 200 kwa kila tiketi.
Nauli ya ndani kwa waamuzi, kamishna na mtathimini wa waamuzi ni sh. 90,000. Posho ya kujikimu kwa kamishna ni sh. 40,000. Gharama ya tiketi ni sh. 1,230,000 wakati usafi na ulinzi ni sh. 500,000.
Baada ya gharama hizo za awali kila klabu ilipata sh. 907,424, gharama za mchezo sh. 302,475, Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu- FDF (sh. 151,237), Uwanja sh. 302,475, DRFA (sh. 120,990) na Baraza la Michezo la Taifa- BMT (sh. 30,247).

Comments