PAPIC AFUNGWA MWAKA MMOJA YANGA

YANGA imeamua kumpa mkataba wa mwaka mmoja kocha wake, Msebia Kostadin Papic.
Habari kutoka ndani ya klabu hiyo yenye maskani yake mitaa ya Jangwani na Twiga zinasema kwamba baada ya mvutano wa muda mrefu juu mkataba wa kocha huyo waliona ni vema wampe mwaka mmoja kwanza.
Kiongozi mmoja wa Yanga amesema kwamba wameamua kumpa muda huo baada ya kujifunza katika msimu uliopita ambapo alitoroka nchi kabla ya muda wake kumalizika huku akiiacha timu ikiwa katika wakati mgumu wa mashjindano.
"Papic ni kocha mzuri lakini ana maamuzi anayoamua kufanya anapojisikia hivyo tumeona tumpe mwaka mmoja kwanza kama akitulia tutamuongeza,"Alisema.

Comments