DU ETI MWENYEKITI WA BMT HAMFAHAMU HENRY JOSEPH LO!

MWENYEKITI wa baraza la Michezo la Taifa (BMT) Dioniz Malinzi juzi aliwaacha vinywa wazi wadau mbalimbali waliohudhuria hafla ya kuagwa kwa timu ya Taifa baada ya kutomfahamu, nahodha wa timu hiyo Henry Joseph na timu anayokipiga.
Katika hafla hiyo, ilipofika kipindi cha kwenda kukabidhiwa bendera, na Henry akikaribia meza eneo la tukio, mwenyekiti huyo alikuwa akiuliza yuko wapi nahodha wa Stars??? huku akiangalia nyuma kabla ya kuelezwa ndio huyo hapo ambapo alimuuliza ndio nani wewe?Henry alipojitambalisha Malinzi tena aliendelea kusema ahh ndo unacheza Sweden?
Du, kwa hali hiyo inaonyesha wazi kuwa mwenyekiti huyo hawafahamu wachezaji hata wa timu hiyo ambayo inaondoka leo kwenda N'Djamena, Chad kwa ajili ya mechi yake ya kuwania mchujo wa kucheza kombe la Dunia.
 Henry anayekipiga katika klabu ya Kongsvinger IL ya  Norway kwa sasa ndiye nahodha wa timu hiyo akirithi mikoa ya Shadrack Nsajigwa ambaye amekuwa akiandamwa na majeruhi hivyo kutoitumikia timu hiyo.

Comments

  1. Kwani ni lazima kuwafahamu wachezaji wote? yeye ni BMT...acheni stori zenu zisizo na kichwa wala miguu.

    ReplyDelete
  2. YANGA BOMBA-UHURU BRANCHNovember 9, 2011 at 8:35 PM

    HAKUNA AJABU YEYOTE HAPO,KUMBUKENI YEYE SIO MWENYEKITI WA BARAZA LA SOKA NI MWENYEKITI WA BARAZA LA MICHEZO KIUJUMLA,SASA ATAMJUA KILA MWANAMICHEZO??? SEMA WATU WA MPIRA KWA MAANA YA SOKA MNAONAGA MICHEZO NI SOKA TU NA HILI NI TATIZO MPAKA KWA WANAHABARI WETU NYIE

    ReplyDelete

Post a Comment