AMIR KHAN ULINGONI DESEMBA 10

LONDON, England

AMIR ‘King’ Khan anatarajiwa kukutana na mbabe Peterson Peterson katika pambano linalotarajiwa kufanyika Desemba 10 mwaka huu.
Hili linakuwa pambano la kwanza kwa mbabe huyo kucheza tangu alipokutana na Marcos ‘Chino’ Maidana katika ukumbi wa Las Vegas, Desemba ya mwaka uliopita na kufanikiwa kuwa bondia wa mwaka.

Wawili hawa watapambana katika pambano la utangulizi litakalowakutanisha wababe wawili wanaowania uzito wa juu wa dunia Wladimir Klitschko na Jean Marc Mormeck.
Akizungumzia pambano hilo mwandaaji wa pambano hilo, Richard Schaefer kutoka kampuni ya Golden Boy Promotions alisema "tunaamini kati ya mapambano hayo mawili, lile la Amir Khan ndilo linatarajiwa kuwa zuri na kubwa kwa siku hiyo."

Comments