MABINGWA watetezi wa ligi kuu soka Tanzania Bara, Yanga wamefuta mapumziko ya siku tatu waliyowapa wachezaji wake na hivyo kuendelea kujifua kwa ajili ya kujiandaa na ligi hiyo.
Yanga ambayo katika katikati ya wiki hii ilipata ushindi mnono kwa kuilamba Coastal Union ya Tanga kwa mabao 5-0, iliamua kuwapa mapimziko wachezaji wake huku ikipanga kuanza kujinoa jumatatu, lakini jana ilisitisha mapumziko hayo.
Msemaji wa Yanga Louis Sendeu alisema jana kwamba wameamua kusitisha mapumziko hayo kutokana na timu kukabiliwa na ushindani mkubwa wa ligi katika mechi zinazofuata.
Alisema ushindi walioupata umewapa changamoto ya kujiandaa zaidi ili kuweza kukabiliana na ushindani wa mechi zinazofuata kwani kila timu imeingiwa na wasiwasi kutokana na kipigo hicho.
Sendeu aliongeza kuwa katika siku ambazo ligi hiyo imesimama wachezaji watakuwa wakifanya mazoezi asubuhi tu katika uwanja wa Taifa, hivyo anaamini timu yake itaendelea kufanya vema katika ligi hiyo.
Comments
Post a Comment