TFF YAJA NA MPANGO WA MAENDELEO

TFF iko katika mchakato wa kutengeneza mpango wa maendeleo wa muda mrefu. Ni nia ya TFF kufanyia kazi maoni ya wadau ili kuhakikisha yanaingia katika mpango huo.

Hivyo wadau wanakaribishwa kutuma maoni yao kupitia email- tfftz@yahoo.com au sanduku la barua 1574 Dar es Salaam. Maoni yawe yametumwa kufikia mwishoni mwa Novemba mwaka huu.
Pia TFF kupitia Kurugenzi ya Ufundi itakutana na makundi mbalimbali kusikiliza maoni yao. Novemba 2 mwaka huu imepanga kukutana na Chama cha Waandishi wa Habari za Michezo Tanzania (TASWA) na pia waandishi wa habari.

Boniface Wambura Mgoyo
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)

Comments

  1. YANGA BOMBA UHURU BRANCHOctober 23, 2011 at 6:37 PM

    WALE WAJUAJI WA WABONGO WANAOJIFANYAGA WANAJUA KUCHAMBUA NA KUKOSOA AKINA SHAFI DAUDA,EDDO KUMWEMBE,SIJUI SAID TULI,MASUDI IBRAHIM,ALLY MAYAI NA WAJUAJI WENGINE WOTE HII NDIO NAFASI SASA KAMA KWELI MNA MAWAZO ENDELEVU YAPELEKENI HUKO ILI YAKISHINDWA KU WORK TUJE TUWACHAMBUE NA NYIE....

    MDAU WA BOMBA - MICHIGAN,US

    ReplyDelete

Post a Comment