STAZ WAONDOKA KESHO KUTWA KUIFUATA MOROCCO

Taifa Stars inatarajiwa kuagwa Oktoba 6 mwaka huu saa 4 asubuhi kambini kwao hoteli ya Chichi iliyoko Kinondoni, Dar es Salaam kabla ya kuondoka siku hiyo hiyo mchana kwenda Casablanca kwa ajili ya mechi dhidi ya Morocco.
 Mechi hiyo ya mwisho ya mchujo kwa ajili ya fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika zitakazofanyika mwakani katika nchi za Equatorial Guinea na Gabon itachezwa Oktoba 9 mwaka huu katika mji wa Marrakech.
Wachezaji wanaocheza nje ya nchi ambao tayari wameripoti Taifa Stars ni Idrissa Rajab anayechezea Sofapaka ya Kenya, Mbwana Samata (TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo- DRC), Henry Joseph (Kongsvinger IL, Norway), Nizar Khalfan (Vancouver Whitecaps, Canada) na Athuman Machupa (Vasalund IF, Sweden).
Washambuliaji Abdi Kassim na Dan Mrwanda wanaocheza mpira wa kulipwa nchini Vietnam wao wanatarajiwa kuwasili nchini leo (Oktoba 4 mwaka huu) saa 8 mchana.

Comments