SIMBA KUINGIA MKATABA WA UJENZI WA UWANJA WAKE MWEZI NOVEMBA

KLABU ya Simba inatarajiwa kuingia mkataba na Kampuni ya Portland ya nchini Uturuki ambayo itajenga uwanja wa kisasa utakaotumiwa na klabu hiyo ‘Simba Sports Arena’ katika eneo la Bunju, nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam Novemba mwaka huu.

Habari zilizopatikana kutoka ndani ya uongozi wa Simba, zinasema kwamba, wawakilishi wa kampuni hiyo wanatarajiwa kutua nchini kati ya Novemba 15 na 18 mwaka huu, kwa ajili ya kuendesha zoezi hilo.
Uwanja huo utakapokamilika utakuwa na uwezo wa kubeba watu 30,000 kwa wakati mmoja, huku pia ukiwa na maduka, migahawa, vituo vya michezo na kumbi za mikutano.

Comments

  1. YANGA BOMBA - UHURU BRANCHOctober 23, 2011 at 6:28 PM

    TAMTHILIA YA DAYZ OF OUR LIVES NAONA BADO INAENDELEA!!!!!ADEN BWANA,ANAWAJUILIA SANA WANYAMA!!AZAM HAWAKUPIGA MAYOWE TULIKUJA KUSHTUKIA TU UWANJA UMEKAMILIKA NA LEO BILA AIBU TUNAENDA KUUCHEZEA UWANJA ULE!!SHAME ON US!

    ReplyDelete

Post a Comment