KUZIONA SIMBA, LYON 15,000

Viingilio katika mechi namba 62 ya Ligi Kuu ya Vodacom kati ya Simba na African Lyon itakayochezwa Oktoba 16 mwaka huu Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam vitakuwa kama ifuatavyo;

VIP A itakuwa sh. 15,000, VIP B sh. 10,000, VIP C sh. 7,000, viti vya rangi ya chungwa (orange straight and curve) sh. 5,000 wakati viti vya kijani na bluu itakuwa sh. 3,000.
Mechi hiyo itaanza saa 10 jioni na tiketi zitauzwa uwanjani kwenye magari maalumu.


LIGI KUU YA VODACOM
Mechi za wiki hii za Ligi Kuu ya Vodacom ni kama ifuatavyo;
Oktoba 15- JKT Ruvu vs Azam (Uwanja wa Chamazi)
Oktoba 16- Simba vs African Lyon (Uwanja wa Taifa)
Oktoba 19- Simba vs Ruvu Shooting (Uwanja wa Chamazi)
Oktoba 20- Yanga vs Toto Africans (Uwanja wa Taifa)
Oktoba 21- Azam vs Polisi Dodoma (Uwanja wa Chamazi)
Oktoba 22- Simba vs JKT Ruvu (Uwanja wa Taifa)
Oktoba 23- Yanga vs Oljoro (Uwanja wa Chamazi)


Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)

Comments