KAMANDA KOVA MGENI RASMI PAMBANO LA MBWANA MATUMLA, MIYEYUSHO

KAMANDA wa polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam ambaye pia ni mlezi wa mchezo wa ngumi nchini, Suleiman Kova anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika pambano la ngumi la kuwania ubingwa wa mabara wa chama cha UBO,linalotarajiwa kufanyika Oktoba 30 kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee, jijini Dar es Salaam.



Pambano hilo la raundi 12 uzito wa Bantam litawakutanisha bingwa Mtetezi Mbwana Matumla atakayezidunda na Francis Miyeyusho.


Mkurugenzi wa Kampuni ya Dar World Link inayoandaa pambano hilo, Muddy Bawazir  amesema leo  klwamba Kamanda Kova amekubali kuwa mgeni rasmi katika pambano hilo ili kuweza kutoa hamasa kwa vijana kuupenda mchezo huo.

Comments