YANGA leo imewapa raha mashabiki wake baada ya kuifumua Coastal Union ya Tanga kwa mabap 5-0 katika mechi ya Ligi Kuu soka Tanzania Bara iliyofanyika kwenye Uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam.
Kwa ushindi huo, Yanga imepanda hadi nafasi ya nne baada ya kufikisha pointi 12, hivyo kuwafukuzia mahasimu wao wa jadi, Simba wanaoongoza kwa pointi 18, wakifuatiwa na Azam yenye pointi 15 na Ruvu Shooting inashika nafasi ya tatu ikiwa na pointi 13.
Comments
Post a Comment