SIMBA YATOKA SALAMA KAITABA, YANGA CHALI KWA AZAM TAIFA

YANGA ya Dar es Salaam imeendelea kusuasua katika Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, baada ya leo kufungwa 1-0 na Azam FC, bao pekee la John Bocco 'Adebayor'. Simba nao wameshindwa kuendeleza wimbi la ushindi baada ya kulazimishwa sare ya kufungana 1-1 na Kagera Sugar Uwanja wa Kaitaba, Bukoba. Simba imezidi kujitanua kileleni baada ya kufikisha pointi 14, wakati Yanga imebaki na pointi zake sita katika mechi sita.

Comments

  1. EEH!WAMEFUKIA MAITI NYINGINE NINI?YANGA MWAKA HUU INAFUNGWA MPAKA NA AZAM AMBAO MARA NYINGI HUWASUMBUA WANYAMA....HII KALI,SINA LA KUSEMA

    ReplyDelete

Post a Comment