POULSEN KUTAJA SILAHA ZA MOROCCO SEPTEMBA 28

Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Jan Poulsen anatarajia Septemba 26 mwaka kutaja wachezaji watakaoingia kambini kwa ajili ya mechi dhidi ya Morocco itakayochezwa Oktoba 9 mwaka huu jijini Casablanca.

Timu inatarajia kuingia kambini Septemba 28 mwaka huu, na inatarajia kuondoka Oktoba 6 mwaka huu kwenda Casablanca. Mechi hiyo ni ya mwisho hatua ya makundi kutafuta tiketi ya kucheza fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika zitakazofanyika mwakani nchini Equatoria Guinea na Gabon.
Poulsen ambaye pia ni Mkufunzi wa Makocha wa Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) yuko nchini Gambia ambapo anaendesha kozi ya wakufunzi na anatarajia kurejea nchini Septemba 24 mwaka huu.

LIGI DARAJA LA KWANZA

Ligi Daraja la Kwanza inayoshirikisha timu 18 inatarajia kuanza mwezi ujao. Kamati ya Mashindano inayoongozwa na Makamu wa Pili wa Rais wa TFF, Ramadhan Nassib inatarajia kukutana Septemba 24 mwaka huu kuangalia mambo mbalimbali ya ligi hiyo.
Moja ya mambo ambayo kamati hiyo itafanya ni kupitisha tarehe ya kuanza ligi hiyo pamoja na vituo.

Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)

Comments