MWANAMUZIKI siku nyingi Kasaloo Kyanga ambaye ni pacha wa mwanamuziki Kyanga Songa amefariki dunia leo katika Hospitali ya Mwananyamala Kinondoni Jijini Dar es Salaam.
Akithibitisha kifo cha mwanamuziki huyo, mmoja ya wakurugenzi wa bendi ya Njenje ambaye aliwahi kufanya kazi na marehemu wakiwa bendi Tuncut Almas, John Kitime, alisema, Kyanga mwenye asili ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) alifariki baada ya kuugua.
Marehemu ameacha mjane na watoto sita ambapo mazishi yake yanatarajiwa kufanyika kesho katika makaburi ya Sinza.
"Ninakwenda safari...safari yenyewe ya masafa marefu...najua hapa unabaki watasema mengi..pia wabaya wetu mama watafurahi"
ReplyDelete"Tunza watoto mama nitarudi..tutaonana kwa mapenzi ya mungu..."
R.I.P. Brother KASALOO KYANGA,machozi yamegubika kope za macho yangu,simanzi moyoni,mbele yetu nyuma yako,najua mengi yatasemwa sana juu ya kifo chako lakini mola ndie anaejua sababu ya kifo chako
mdau yanga bomba,U.S.A.