KAIJAGE AIBUKIA UWAKALA WA WACHEZAJI FIFA

Mtihani wa uwakala wa wachezaji (players agent) wa Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) umefanyika leo (Septemba 29 mwaka huu) saa 4 asubuhi kwenye ofisi za Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF). 
Watanzania wanane walijisajili kwa ajili ya kufanya mtihani huo. Watano kati ya hao ndiyo wamejitokeza na kufanya mtihani huo ambao ulikuwa na sehemu mbili. Maswali kutoka FIFA na mengine kutoka TFF.
 Walioomba uwakala na kufanya mtihani huo ni Adam Kapama, Aziz Sharif, Dk. Cyprian Maro, Florian Kaijage na Valence Mayenga. Mtihani mwingine wa uwakala utafanyika Machi mwakani.
 Mpaka sasa Tanzania ina mawakala saba wa wachezaji wanaotambuliwa na FIFA. Mawakala hao ni Ally Mleh wa Manyara Sports Management, Damas Ndumbaro, John Ndumbaro, Mehdi Remtulla, Ally Saleh, Yusuf Bakhresa na Said Tully. 

Comments