Fabio Capello amekiri England ilikuwa na bahati kushinda dhidi ya Wales matokeo yaliyoiweka katika nafasi ya kufuzu kwa mashindano ya nchi za Ulaya yaitwayo Euro fainali zake zitakazofanyika mwaka 2012 na akadai wachezaji wake wanakuwa hawajiamini wanapocheza katika uwanja wa Wembley.
Bao la Ashley Young katika dakika ya 35 limeipa England ushindi wa kwanza katika uwanja wa Wembley kwa zaidi ya mwaka mmoja na sasa wanahitaji pointi moja tu katika mchezo wao wa mwisho watakapokumbana na Montenegro mwezi ujao ili iweze kusonga mbele katika fainali zitakazochezwa Poland na Ukraine.
Capello alisema: "Tulikuwa na bahati. Wakati mchezaji wao alipofanya makosa makubwa mbele ya lango ilikuwa bahati kwetu, lakini naona hatukucheza vizuri sana katika dakika 15 za mwisho na tulikuwa tunahaha.
"Tulicheza vizuri sana kwa dakika 20 kipindi cha kwanza, lakini tunahitajika kucheza vyema kwa muda wote wa mchezo."
Comments
Post a Comment