ARSENE WENGER amesema hatajiuzulu Arsenal pamoja na kipigo cha mbwa mwizi kutoka kwa Manchester United. The Gunners walikung'utwa 8-2 kwenye Uwanja wa Old Trafford leo, lakini Wenger, ambaye anasherehekea miaka 15 kazini mwezi ujao, alisema: "Naamini tuna mapumziko kabla ya mechi ijayo,". kuhusu kujiuzulu, alisema; "Hapana, hapana kabisa."Wenger ameshuhudia Nahodha wake Cesc Fabregas akitimkia Barcelona na Samir Nasri na Gael Clichy wamejiunga na Manchester City, wakati kocha huyo Mfaransa amewasajili Gervinho na Alex Oxlade-Chamberlain, ingawa mashabiki wa Gunners wanataka sura mpya zaidi.
Lakini Wenger amesistiza kutumia fedha haliwezi kuwa jibu la matatizo ya Arsenal.
Lakini Wenger amesistiza kutumia fedha haliwezi kuwa jibu la matatizo ya Arsenal.
Comments
Post a Comment